Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 13:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Wakati huo hakukuwa mufuaji yeyote wa vyuma katika inchi nzima ya Israeli, maana Wafilistini walikusudia kuwazuia Waebrania wasipate kujitengenezea mapanga au mikuki.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 13:19
6 Σταυροειδείς Αναφορές  

Alitwaa watu wote wa Yerusalemu: wakubwa wote, watu wote waliokuwa mashujaa, wafungwa elfu kumi, na wafundi wote na wafuaji wa vyuma. Hakuna aliyebaki isipokuwa wale waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi.


Mimi ndiye niliyemwumba mufuaji wa vyuma, anayewasha moto wa makaa na kufua silaha. Ni mimi vilevile niliyemwumba mwangamizaji anayeangamiza.


Ilikuwa nyuma ya Nebukadneza mufalme wa Babeli kuwahamisha Yekonia mufalme wa Yuda mwana wa Yoyakimu, pamoja na wakubwa wa inchi ya Yuda na wafundi bora na wafuaji wa vyuma kutoka Yerusalema na kuwapeleka Babeli. Yawe akanionyesha vikapu viwili vya matunda ya tini vimewekwa mbele ya hekalu la Yawe.


Wakati huu ulikuwa nyuma ya kuondoka Yerusalema kwa mufalme Yekonia na malkia mama wa mufalme, matowashi wa mufalme, wakubwa wa inchi ya Yuda na wa Yerusalema, wafundi na wafua vyuma.


Walijichagulia miungu mipya, kukakuwa vita katika inchi. Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao kati ya watu elfu makumi ine wa Israeli.


Kila Mwisraeli alilazimishwa kuwaendea Wafilistini kunoa majembe yake au sururu au shoka au kisu cha kuvuna.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις