Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 12:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini wao walimusahau Yawe, Mungu wao, naye akawatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa waaskari wa muji wa Hazori, na katika mikono ya Wafilistini na katika mikono ya mufalme wa Moabu. Mataifa hayo yalipigana na babu zenu na kuwashinda.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 12:9
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakulinda kutokana na waadui zako wote. Zaidi ya hayo, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakujengea nyumba.


Walimusahau Mungu aliyewaokoa, aliyetenda mambo makubwa katika inchi ya Misri,


Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.


Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?


Hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli, naye akawatia katika mikono ya Wafilistini na Waamoni.


Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe, naye akawaacha watawaliwe na Wafilistini kwa miaka makumi ine.


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wanyanganye mali zao. Akawatoa kwa waadui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwashinda.


Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe. Yawe akamutia nguvu mufalme wa Moabu aliyeitwa Mwana-Ngombe kusudi awashambulie Waisraeli, kwa sababu walitenda uovu mbele ya Yawe.


Nyuma ya Ehudu mwana wa Anati, Samugari akakamata nafasi yake. Yeye aliwaua Wafilistini mia sita kwa fimbo ya kuchunga ngombe. Naye vilevile aliwakomboa Waisraeli.


Yawe akawatia katika mikono ya mufalme wa Kanana, jina lake Asikie, ambaye aliishi Hazori. Jemadari wa waaskari wake aliitwa Sisera, mukaaji wa Haroseti-Hagoimu.


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις