Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Roho wa Yawe atakufikia kwa nguvu, nawe utaanza kutabiri pamoja nao na kugeuka kuwa mutu mwingine.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 10:6
14 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.


Hapo, Yawe akashuka katika wingu na kuzungumuza naye. Halafu akatwaa sehemu ya roho aliyokuwa amemupa Musa, akawapa kila mumoja wa wale wazee makumi saba. Walipoingiwa na roho huyo, wazee hao wakaanza kutoa unabii, lakini hawakurudia kufanya hivyo.


Wazee wawili kati ya wale makumi saba waliochaguliwa, Eldadi na Medadi, walikuwa wamebaki katika kambi wenzao walipokwenda kwenye hema. Roho iliwafikia humohumo ndani ya kambi, wakaanza kutoa unabii pahali walipokuwa.


Lakini Musa akamujibu: Unaona wivu kwa ajili yangu? Heri Yawe angewapa watu wake wote roho yake nao wapate kuwa manabii!


Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’


Basi, roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, akamurarua simba huyo kama mutu anavyorarua mwana-mbuzi. Naye Samusoni hakuwaambia wazazi wake jambo lile.


Alipofika Lehi, Wafilistini wakamwendea mbio na walikuwa wanapiga kelele. Kwa rafla roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu na zile kamba walizomufunga kwenye mikono yake zikakatika kama kitani kilichoguswa na moto, navyo vifungo vikaanguka chini.


Basi, roho wa Yawe akamujaza Otinieli, naye akakuwa mwamuzi wa Waisraeli. Otinieli alikwenda katika vita naye Yawe akamutia Kusani, Yule-Mwovu-Sana, ufalme wa Mesopotamia, katika mikono yake.


Saulo na mutumishi wake walipofika kule Gibea, alipokelewa na kundi la manabii. Roho wa Mungu alimufikia kwa nguvu, na Saulo akaanza kutabiri pamoja na manabii hao.


Saulo alipogeuka kwa kumwacha Samweli, Mungu akabadilisha moyo wa Saulo. Yale yote aliyoambiwa na Samweli yakatokea siku hiyo.


Mara moja, Saulo aliposikia maneno hayo, roho wa Mungu akamufikia kwa nguvu, naye akawaka hasira kali.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Kwa hiyo Saulo akatuma watu kwenda kumukamata. Lakini walipokuta kundi la manabii likitabiri na Samweli akiliongoza, Roho wa Mungu aliwafikia wale watumishi wa Saulo, nao vilevile wakaanza kutabiri.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις