Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.
Usimwangalie Nabali ambaye ni mutu mubaya. Maana jina lake la Nabali linamustahili. Yeye anaitwa Nabali; na kweli yeye ni mutu mupumbafu. Bwana wangu, wale vijana wako ulipowatuma, mimi mujakazi wako sikuwaona.