Muhubiri 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Nilifikiri sana juu ya hayo yote, nikaona kwamba Mungu anaongoza matendo ya watu wenye hekima na wenye haki; ikiwa ni upendo au chuki, mwanadamu hajui. Kila kitu kwao ni bure, 2 maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa. 3 Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa. 4 Lakini anayeambatana na wanaoishi angali bado na tumaini. Afazali imbwa mwenye kuishi kuliko simba mwenye kufa. 5 Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa. 6 Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua. 7 Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako. 8 Vaa vizuri, ujipakae mafuta kwenye kichwa. 9 Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua. 10 Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda. Hasara inakuja kwa rafla 11 Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja. 12 Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia. 13 Vilevile hapa chini ya jua nimeona mufano wa hekima, na ulionekana kwangu kuwa wenye maana sana. 14 Kulikuwa muji mumoja mudogo wenye wakaaji wachache. Mufalme mumoja mwenye nguvu akafika, akauzunguka na kujitayarisha kuushambulia. 15 Katika muji ule, kulikuwa masikini mumoja mwenye hekima ambaye, kwa hekima yake, aliokoa muji ule. Lakini hakuna mutu aliyemukumbuka yule masikini kisha. 16 Basi, mimi ninasema, hekima ni bora kuliko nguvu, ingawa hekima ya masikini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwi. 17 Afazali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima, kuliko kusikiliza kelele za mufalme katika kikao cha wapumbafu. 18 Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo