Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -

Muhubiri 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”

2 Kwa wakati huu wa nyuma, jua, mwangaza, mwezi na nyota hazionekani tena, mawingu yanarudia nyuma ya mvua,

3 walinzi wa nyumba wanatetemeka, wenye nguvu wanakunjama, wasagaji wanaacha kazi kwa sababu ni wachache, wanaochungulia kwenye dirisha wanakuwa zaifu,

4 milango imefungwa, sauti za visagio zimekuwa ndogo, watu wanashituliwa na sauti ya ndege, sauti za muziki zimekuwa ndogo,

5 watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,

6 uzi wa feza unakatika kikombe cha zahabu kinapondekana, mutungi wa maji unavunjikia kwenye chemichemi, gurudumu la kukokota maji linavunjika kwenye kisima,

7 mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.

8 Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.


Maneno ya mwisho

9 Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.

10 Muhubiri alijikaza kupata maneno ya kupendeza, akaandika kwa usawa maneno ya kweli.

11 Misemo ya wenye hekima ni kama fimbo ya kuongoza ngombe. Mezali zilizokusanywa pamoja na muchungaji mumoja ni kama misumari iliyopigiliwa kwa nguvu.

12 Zaidi ya hayo, mwana wangu, ujilinde! Kuandika vitabu hakuna mwisho na kusoma kwingi kunachokesha mwili.

13 Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.

14 Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Volg ons:



Advertensies