Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Waebrania 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kule babu zenu walinipima na kunijaribia, ingawa walikuwa wameona yote niliyotenda kwa muda wa miaka makumi ine.

Sien die hoofstuk Kopieer




Waebrania 3:9
17 Kruisverwysings  

Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu


Waisraeli waliponililia mimi Yawe, niliweka giza kati yao na Wamisri na kuifanya bahari iwafunike Wamisri. Ninyi wenyewe mulijionea yale niliyowatendea Wamisri. Muliishi katika jangwa muda murefu.


Wakati huo wa miaka makumi ine nguo zenu hazikuchakaa, wala miguu yenu haikuvimba.


Ninyi muliona kwa macho yenu mambo ambayo Yawe aliyafanya juu ya Bali-Peori. Yawe, Mungu wenu, aliwaangamiza watu wote kati yenu waliomwabudu huyo mungu Bali-Peori.


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


Lakini yule muchawi Elema, (kufuatana na maana ya jina lake katika Kigriki), akapingana nao, akitaka kumugeuza yule liwali kusudi asiamini Neno la Mungu.


Halafu Yesu akawajibu wale wajumbe: “Mwende kumwelezea Yoane mambo muliyoona na kusikia: vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Ninyi mumeona mambo yote Yawe, Mungu wenu, aliyoyatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu. Yawe, Mungu wenu, ndiye aliyewapigania.


Muliona majaribu makubwa, vitambulisho na maajabu aliyotenda.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Watoto wenu watatangatanga na kutaabika humu katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine kwa ajili ya ukosefu wenu wa imani mpaka mutu wenu wa mwisho atakapokufia katika jangwa.


Yawe akamwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.


Waisraeli walisafiri kwa muda wa miaka makumi ine katika jangwa hata wanaume wote waliokuwa na umri wa kwenda kwa vita wakaangamia kwa kuwa hawakusikiliza mambo Yawe aliyosema. Yawe alikuwa amewaapia watu hao kwamba hawataiona inchi ile inayotiririka maziwa na asali ambayo yeye aliwaapia baba zao kwamba atawapa.


Maana macho yenu yameona matendo yote haya makubwa ambayo Yawe alifanya.


babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies