Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 9:3
30 Kruisverwysings  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


kefu sasa mwanadamu anayekuwa chukizo na mupotovu, mwanadamu anayetenda uovu kama kunywa maji!


Hata hivyo, wote wanakufa na kuzikwa, wote wanafunikwa na vidudu.


Yote ni mamoja, kwa hiyo ninasema: Mungu anawaangamiza wakamilifu na waovu.


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Wanafanya shauri baya wakijisemesha: “Tumetimiza sasa mipango yetu! Nani anayeweza kugundua mafikiri ya ndani ya mutu?”


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.


Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa.


Lakini anayeambatana na wanaoishi angali bado na tumaini. Afazali imbwa mwenye kuishi kuliko simba mwenye kufa.


Ninyi mumefanya vibaya zaidi kuliko babu zenu, maana kila mumoja wenu ni mwenye moyo mugumu na mwenye nia mbaya, wala hamunisikilizi.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Basi akaanza kufikiri yeye mwenyewe na kujisemesha: ‘Watumishi wote wa baba yangu wana vyakula kwa uwingi, nami huku ninakufa na njaa!


Lakini wale wakubwa wakakasirika sana, wakaanza kusemezana wao kwa wao juu ya namna watakavyomutendea Yesu.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Mara nyingi niliwaazibu katika nyumba za kuabudia na kuwashurutisha wakane imani yao. Niliwakasirikia kupita kipimo, hata nikaenda kuwatesa katika miji ya inchi za kigeni.


Paulo alipokuwa akijitetea vile, Festo akamwambia kwa sauti kubwa: “Wewe Paulo, uko na wazimu! Elimu yako nyingi imekuvuruga kichwa.”


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


lakini alikaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Basi punda, ambaye hasemi, alisema kama mutu na kuzuiza kitendo cha upumbafu wa yule nabii.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies