Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 8:12
34 Kruisverwysings  

Hakuna mutu aliyekusudia kutenda maovu mbele ya Yawe kama Ahabu, ambaye alishawishiwa na Yezebeli, muke wake.


Ee dunia yote; tetemeka mbele yake! Ameweka ulimwengu imara, hautatikisika.


Sasa, kwa vile Mungu anazuia hasira yake, wala hajali sana makosa ya watu,


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata uheri.


Lakini wapole watarizi inchi, hao wataifurahia amani kamili.


Mumwabudu Yawe katika pahali pake patakatifu; tetemeka mbele yake, ee dunia nzima!


Basi, Mungu akawajalia mema wazalishaji wale, nao Waisraeli wakazidi kuongezeka na kuwa na nguvu sana.


Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.


Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.


Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.


Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Mpaka hivi leo hamujajinyenyekeza wala kuogopa wala kuzifuata sheria zangu na masharti yangu nilizowawekea ninyi na babu zenu.


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Basi kuna nini? Mungu alitaka kuonyesha kasirani yake na kutambulisha uwezo wake. Lakini aliwavumilia sana wale waliostahili kupatwa na kasirani yake na waliokuwa wametayarishwa kwa kuangamizwa.


Musikule damu, nanyi mutafanikiwa pamoja na wazao wenu, maana mutakuwa munatenda kwa usawa mbele ya Yawe.


Mufanye angalisho kutii maneno haya niliyowaamuru, kusudi mupate kufanikiwa ninyi pamoja na wazao wenu nyuma yenu milele, maana mutakuwa munatenda mazuri na kwa usawa mbele ya Yawe, Mungu wenu.


Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”


Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies