Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 7:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mwisho wa jambo ni afazali kuliko mwanzo wake. Moyo muvumilivu ni bora kuliko moyo wa majivuno.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 7:8
20 Kruisverwysings  

Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.


Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.


Asiyekuwa mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu. Anayetawala nafsi yake ni bora kuliko anayetaka muji.


Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.


Sifa nzuri ni bora kuliko marasi ya bei kali. Siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.


Lakini Abrahamu akamujibu: ‘Mutoto wangu, kumbuka kwamba umekwisha kupewa mema yaliyokupasa wakati ulipoishi katika dunia, na Lazaro alipata taabu. Na sasa yeye anatulizwa, lakini wewe unateswa.


Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema.


Nanyi vilevile, muvumilie na kutia mioyo yenu nguvu, kwa maana Bwana yuko karibu kurudi.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies