11 Hekima ni ya bei kubwa kama urizi; ni ya mafaa kwa wale wote wanaokuwa wazima.
Lakini hekima itapatikana wapi? Ni pahali gani panapopatikana maarifa?
Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.
Mali ni taji ya utukufu wa wenye hekima, lakini ujinga ni kitambaa cha wapumbafu.
Hekima ni bora kuliko feza, ina faida kuliko zahabu.
Hekima ni ya maana sana kuliko mawe ya bei kali, hakuna kitu unachotamani kinachoweza kulingana nayo.
Mwangaza ni muzuri, na kuona jua kunapendeza macho.
Basi, mimi nikagundua kwamba hekima ni bora kuliko upumbafu, kama vile mwangaza unavyokuwa bora kuliko giza.
Usiulize: “Kwa nini nyakati za zamani zilikuwa bora kuliko za sasa?” Hauulizi hivyo kwa kutumia hekima.