Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.
Gideoni akamwambia: “Ee Bwana wangu, ikiwa Yawe yuko pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu ambayo wazee wetu walituelezea, wakisema: ‘Yawe ndiye aliyetutoa katika inchi ya Misri.’ Lakini sasa Yawe ametutupilia na kututia katika mikono ya Wamidiani!”