Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Angalia kinywa chako kisikuingize katika zambi, halafu ikupase kumwambia mujumbe wa Mungu kwamba haukukusudia kutenda zambi. Kwa nini kumusukuma Mungu akukasirikie na kuiharibu kazi yako?

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 5:5
8 Kruisverwysings  

Ni hatari kusema kwa muzaha “Nitamutolea Mungu hiki!” na kuanza kufikiri nyuma ya kufanya naziri ile.


Au, kama mutu akiapa kufanya kitu chochote, chema au kibaya, kama vile watu wanavyofanya bila kufikiri, atakapojua atakuwa na kosa.


Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure, wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Mbele haujauzisha lile shamba, si lilikuwa mali yako? Na nyuma ya kuliuzisha, feza ulizopata haungezitumia sawa unavyotaka? Basi namna gani ulikusudia kufanya jambo kama hili? Haukusema uongo mbele ya watu, lakini mbele ya Mungu!”


Unaweza kuomba faida unapomukopesha mugeni, lakini ndugu yako Mwisraeli usimulipishe faida, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki katika shuguli zako zote utakazofanya katika inchi ambayo unakwenda kurizi.


Unapofanya kiapo mbele ya Yawe, Mungu wako, usichelewe kukitimiza, maana Yawe, Mungu wako, atakidai kwako, nawe utakuwa na kosa.


Yefuta alipomwona, akapasua nguo yake kwa huzuni na kusema: “Ee binti yangu! Umenivunja moyo. Wewe umekuwa chanzo kikubwa cha matatizo kwangu. Nimekwisha kumwapia Yawe nami siwezi kuvunja kiapo changu.”


Volg ons:

Advertensies


Advertensies