Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 3:8
19 Kruisverwysings  

Inchi yote upande wa magaribi wa muto Furati, kutokea Tifusa mpaka muji wa Gaza, ilikuwa chini ya utawala wake. Wafalme wote upande wa magaribi wa muto Furati walikuwa chini yake, na alikuwa na amani na inchi zote jirani.


Wakati Yoramu alipomwona Yehu, alimwuliza: “Yehu, unakuja kwa amani?” Yehu akamujibu: “Amani gani, wakati makahaba na wachawi wa Yezebeli ni wengi?”


Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.


sitavumilia hata kidogo mambo ya upuuzi. Ninachukia matendo ya watu wapotovu, mimi sitaambatana nayo.


Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake, wakawatendea watumishi wake vibaya.


Ee Yawe, ninawachukia wanaokuchukia; ninawazarau sana wale wanaokuasi!


Mwenye haki anachukia uongo, lakini mwovu anatenda kwa kupatisha haya na mazarau.


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


“Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile.


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Nanyi waume muwapende wake wenu sawa vile Kristo alivyopenda kanisa na kutoa uzima wake kwa ajili yake.


Kwa njia hii wataweza kuwafundisha vijana wanawake kuwapenda waume wao na watoto wao,


Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.


Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies