Sanduku la Yawe lilipokuwa linaingia katika muji wa Daudi, Mikali binti wa Saulo alichungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele ya Yawe. Basi, akamuzarau ndani ya moyo wake.
Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.
Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.
Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.
Basi, huzuni inayosababishwa na Mungu inamuwezesha mutu kugeuka toka katika zambi. Na kugeuka kule, kunamuletea kuokoka. Kule kuokoka hakuleti majuto. Lakini huzuni inayosababishwa na mwanadamu inaleta kifo.