Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 3:3
21 Kruisverwysings  

Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme, ukuwe na mamlaka ya kuongoa na kubomoa, mamlaka ya kuharibu na kuangamiza, mamlaka ya kujenga na ya kupanda mbegu.


Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwaongoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kwa kuwapanda na kuwajenga. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.


Lakini Yawe ameniambia nikuambie: Yawe anasema hivi: Yale niliyojenga ninayabomoa, na yale niliyopanda ninayaongoa; nitafanya hivyo katika inchi yote.


Nitaubomoa kabisa huo ukuta mulioupakaa chokaa, na musingi wake utakuwa wazi. Ukuta huo ukianguka, mutaangamia chini yake. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu hawa wanasema kwamba wakati wa kuijenga upya nyumba ya Yawe haujafika.


Ni sawa kwenu kukaa katika nyumba zenu nzuri wakati nyumba yangu ni mabomoko matupu?


Halafu yule malaika wa Yawe akasema: Ee Yawe wa majeshi, kwa muda gani utaendelea kutokuwa na huruma juu ya muji Yerusalema na miji ya inchi ya Yuda ambayo umeikasirikia kwa muda wa miaka makumi saba?


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.


Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies