Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa,

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 3:2
36 Kruisverwysings  

Lakini agano langu litasimama kwa Isaka ambaye Sara atakuzalia katika mwaka kwa wakati kama huu.”


Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,


Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Elisha akamwambia: “Mwaka kesho, kwa wakati kama huu, utakuwa na mutoto katika mikono yako.” Mama akamujibu: “Hapana, Bwana wangu! Wewe ni mutu wa Mungu; usinidanganye mimi mutumishi wako!”


Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.


Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa. Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake; hawezi kupita mupaka uliomwekea.


Mwanadamu ana magumu katika dunia, na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara!


Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia!


Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri, unapenda uongo kuliko ukweli.


Kwanza fanya kazi zako inje na kutayarisha kila kitu katika shamba. Kisha jenga nyumba yako.


Mulimaji anayetaka kupanda mbegu anaendelea kulima tu siku zote? Anaendelea kutipua na kusawanisha shamba lake?


Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.


Kwenda umwambie Hezekia kwamba: Mungu wa baba yako Daudi, anasema hivi: Nimesikia ombi lako na nimeyaona machozi yako. Basi, ninakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi.


Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.


Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme, ukuwe na mamlaka ya kuongoa na kubomoa, mamlaka ya kuharibu na kuangamiza, mamlaka ya kujenga na ya kupanda mbegu.


Lakini Yawe ameniambia nikuambie: Yawe anasema hivi: Yale niliyojenga ninayabomoa, na yale niliyopanda ninayaongoa; nitafanya hivyo katika inchi yote.


Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.


Yesu akajibu: “Wao ni kama mumea usiopandwa na Baba yangu wa mbinguni, utakaopaswa kuongolewa.


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”


Hata Elizabeti wa jamaa yako, amepata mimba, naye atazaa mutoto mwanaume, ijapokuwa yeye ni muzee. Yeye aliyekuwa akiitwa tasa, sasa huu ni mwezi wa sita wa mimba yake.


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.


“Siku za kutimiza ahadi Mungu aliyotoa kwa Abrahamu zilipokaribia, hesabu ya watu wa taifa letu kule Misri ikaongezeka hata ikazidika sana.


Na katika siku zile Musa akazaliwa, naye alikuwa mutoto muzuri sana. Alilelewa muda wa miezi mitatu katika nyumba ya baba yake.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Basi, Musa mutumishi wa Yawe akakufa kule katika inchi ya Moabu kulingana na neno Yawe alilosema.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele, sasa wanafanya kazi wapate chakula. Lakini waliokuwa na njaa, sasa hawana njaa tena. Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba. Lakini mama mwenye watoto wengi, sasa ameachwa bila mutoto.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies