9 Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.
Heri kwa wake zako! Heri kwa hawa watumishi wako ambao wanakutumikia siku zote na kusikiliza hekima yako!
Alitunga mezali elfu tatu na nyimbo elfu moja na tano.
Hizi ni mezali za Solomono mwana wa Daudi mufalme wa Israeli.
Hizi ni mezali za Solomono: Mutoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake; lakini mutoto mupumbafu ni huzuni ya mama yake.
Hizi nazo ni mezali nyingine za mufalme Solomono zilizoandikwa na watu wa Hezekia, mufalme wa Yuda.
Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.