4 Anayechunguza upepo hatapanda mbegu, anayeangalia mawingu yatoweke, hatavuna kitu.
Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.
Muvivu anasema: “Kuna simba inje. Nitauawa katika njia.”
Usimunyime mutu anayehitaji musaada, ikiwa una uwezo wa kufanya hivyo.
Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha. Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini, pale unapoangukia ndipo unapolala.
Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.