Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 11:2
22 Kruisverwysings  

Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Atakuokoa mara sita toka katika magumu; hata mara saba hasara haitakugusa.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Kuna vitu sita Yawe anavyochukia, hata saba ambavyo ni chukizo kwake:


Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha. Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini, pale unapoangukia ndipo unapolala.


Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


Yesu akamujibu: “Hapana, sikuambii kwamba umusamehe mara saba tu, lakini mpaka mara makumi saba mara saba.


Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.


Kama akikukosea mara saba kwa siku, na akirudia kwako kila mara kwa kukuomba huruma, umusamehe.”


Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.


Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.


Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


Volg ons:

Advertensies


Advertensies