Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yaliyokuwa ndiyo yatakayokuwa, yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka. Chini ya jua hakuna jambo jipya.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 1:9
10 Kruisverwysings  

Watu wanasema: “Angalia jambo hili ni jipya”, kumbe limekwisha kutendeka zamani za kale.


Basi, nikaanza kufikiri maana ya kuwa na hekima, kuwa mwenda-wazimu, na kuwa mupumbafu. Nikajiuliza: “Mufalme mupya anaweza kufanya kitu gani? Atafanya tu kile kilichofanywa mbele yake.”


Kinachotukia sasa, kilikwisha tukia; kitakachotukia nyuma kilikwisha kutukia. Mungu anafanya kitu kitukie tena na tena.


Kila kitu kinachotukia kilikwisha kupangwa tangu zamani. Hali ya mwanadamu inajulikana, na tunajua kwamba muzaifu hawezi kubishana na mutu mwenye nguvu zaidi.


Usiulize: “Kwa nini nyakati za zamani zilikuwa bora kuliko za sasa?” Hauulizi hivyo kwa kutumia hekima.


Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.


Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.


Zamani manabii wa uongo walitokea kati ya watu, na ndivyo hivyo walimu wa uongo watakavyotokea kati yenu. Watu hawa wataingiza mafundisho mabaya sana ya uongo kwa siri, wakimukataa hata Bwana aliyewakomboa na kujiletea maangamizi upesi.


Kisha nikaona mbingu mupya na dunia mupya. Kwa sababu mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimekwisha kutoweka, bahari nayo haikukuwa tena.


Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”


Volg ons:

Advertensies


Advertensies