Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Upepo unavuma tokea kusini, unazunguka mpaka kaskazini. Unazungukazunguka katika mwendo wake, kisha unarudia tena katika muzunguko wake siku zote.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 1:6
11 Kruisverwysings  

Wewe unajiona umevaa nguo za joto sana, wakati upepo wa kusini unapovuma juu ya inchi.


Zoruba inavuma kutoka chumba chake, na baridi kali kutoka katika gala yake.


Aliamuru, akavumisha zoruba kali, ikarusha juu mawimbi ya bahari.


Alituliza ile zoruba kali, nayo mawimbi yakanyamaza.


Mito yote inatiririkia ndani ya bahari, lakini bahari haijai hata kidogo; kule ambako mito inatiririkia ndiko kule inaendelea kwenda.


Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.


Lakini Yawe akavumisha upepo mukali katika bahari, kukatokea zoruba kali. Mashua ikakuwa karibu kuvunjika kabisa.


“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.


Mvua ikanyesha, mito ikajaa, upepo ukavuma na kupiga nyumba ile, nayo ikaanguka na kubomoka kabisa.”


Upepo unavuma pahali unapotaka, nawe unasikia sauti yake, lakini haujui pahali unapotoka wala unapokwenda. Na ni vile inavyokuwa kwa kila mutu anayezaliwa kwa Roho.”


Volg ons:

Advertensies


Advertensies