Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure!

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 1:2
23 Kruisverwysings  

Mupumbafu hawezi kuwa na maarifa. Punda wa pori ni punda wa pori tu.


Mwanadamu ni kama pumzi tu; siku zake zinapita kama kivuli.


Ee Yawe, utajificha hata milele? Mpaka wakati gani hasira yako itawaka kama moto?


Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.


Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.


Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.


Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Yatakayomupata mupumbafu yatanipata na mimi vilevile. Kwa nini, basi, nimekuwa na hekima zaidi?” Nikasema ndani ya moyo wangu: “Hayo nayo ni bure.”


Kwa hiyo, nikachukia maisha, maana yote yanayotendeka chini ya jua yalinisikitisha. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Tena, ni nani anayejua kwamba atakuwa mwenye hekima au atakuwa mupumbafu? Hata hivyo, yeye atarizi yote niliyofanya kwa kutoa jasho na kutumia hekima yangu hapa chini ya jua. Hayo nayo ni bure.


Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.


Maisha yake yote yamejaa taabu, na jasho yake ni mahangaiko matupu. Hata usiku akili yake haipumziki! Hayo nayo ni bure.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nilijikusanyia feza na zahabu kutoka hazina za wafalme na toka katika majimbo, nami nilipata waimbaji wanaume na wanawake, na wahabara wanaotamaniwa.


Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.


Hesabu ya watu haikukuwa na mwisho, naye aliwatawala wote. Hata hivyo, wale wanaozaliwa nyuma hawatamufurahia. Hakika hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Mali ikiongezeka, wale watakaoikula wanaongezeka vilevile, naye mwenye mali inamufalia nini isipokuwa kuiangalia tu mali yake?


Maneno yanapokuwa mengi, ndivyo yanaendelea kuwa bure. Hayana faida.


Kwa maana viumbe vyote vimewekwa chini ya utawala wa mambo ya ovyo, si kwa mapenzi yao, lakini kwa sababu ya yule aliyewatia katika hali hiyo. Lakini kungali tumaini hili:


Volg ons:

Advertensies


Advertensies