Muhubiri 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Basi, nikafikiri nikisema: “Nimejipatia hekima nyingi zaidi kupita wote waliopata kutawala Yerusalema mbele yangu. Kweli, ninajua hekima na maarifa ni nini.”
Lakini sikuweza kuamini habari hizo mpaka nilipofika na kujionea mwenyewe. Kumbe sikuambiwa hata nusu yake; hekima yako na fanaka zako vimepita habari nilizopewa.
Gehazi, mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu, akasema: “Bwana wangu amemwachilia Namani wa Aramu aende bila kupokea chochote alicholeta. Kama vile Yawe anavyoishi, nitamufuata kusudi nipate kitu kutoka kwake.”
Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Yatakayomupata mupumbafu yatanipata na mimi vilevile. Kwa nini, basi, nimekuwa na hekima zaidi?” Nikasema ndani ya moyo wangu: “Hayo nayo ni bure.”
Wewe unayesema: Nitajijengea nyumba kubwa, yenye vyumba vikubwa vya magorofi. Kisha unaifanyia madirisha, ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi, na kuipaka rangi nyekundu!
Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.