Biblia Todo Logo
Aanlyn Bybel

- Advertensies -




Muhubiri 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.

Sien die hoofstuk Kopieer




Muhubiri 1:13
22 Kruisverwysings  

Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


Wachimba madini wanaleta taa katika giza, wanatafutatafuta mpaka chini zaidi ya udongo, na kuchimbua mawe yenye madini katika giza.


Matendo ya Yawe ni makubwa sana! Wote wanaoyafurahia wanayachunguza.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Mutu mwenye akili anajipatia maarifa; sikio la mwenye hekima linatafuta maarifa.


Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu, ufuate mwenendo wa maisha yangu.


Mungu anatukuzwa kwa kuficha mambo, lakini wafalme wanatukuzwa kwa kuchunguza mambo.


Jambo la musingi ni kujipatia hekima; toa vyote unavyokuwa navyo ujipatie akili.


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.


Zaidi ya hayo, mwana wangu, ujilinde! Kuandika vitabu hakuna mwisho na kusoma kwingi kunachokesha mwili.


Maisha yake yote yamejaa taabu, na jasho yake ni mahangaiko matupu. Hata usiku akili yake haipumziki! Hayo nayo ni bure.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Mimi nimeiona kazi ambayo mwanadamu amepewa na Mungu.


Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Ufikiri sana juu ya mambo hayo na ujitolee kwa kuyatimiza hata watu wote waone waziwazi maendeleo yako.


Volg ons:

Advertensies


Advertensies