Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.
Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.
Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.
Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.